Waziri wa habari utamaduni utalii na michezo wa
serikali ya Mapinduzi Zanzibar Rashid Ali Juma amewataka wachezaji waliopo
katika timu ya taifa ya Zanzibar ( Zanzibar Heroes) kujituma kwa moyo wao wote
ilikuviletea heshima visiwa vya Zanzibar.
Waziri wa habari utamaduni utalii na michezo Rashid Ali akizungumza na wachezaji wa Zanzibar Heroes hawapo pichani. |
Waziri Rashid ameyasema hayo wakati alipokuwa
akizungumza na wachezaji wa timu hiyo wakati alipotembelea katika mazoezi ya
timu hiyo.
Baadhi ya wachezaji wakimsikiliza waziri wa habari. |
Ameongeza kuwa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar
kupitia wizara ya habari utamaduni na michezo na baraza la michezo watatoa
ushirikiano wao wa hali na mali ilikuifanya timu hiyo kuwa na maandalizi
yakutosha.
Nae katibu wa
chama cha mpira wa miguu visiwani hapa Muhamed Ali Hilal Tedy amesema chama
chao kimejipanga kuona wanaindaa timu hiyo katika mazingira yaliyo bora.
Amesema changamoto kuu ambayo kwa sasa wanakabiliana
nayo nikukosekana kwa baadhi ya wachezaji ambao wanacheza ligi kuu Tanzania
bara sambamba na ukata wa fedha.
Waziri wa habari akiwa na mwenyekiti wa baraza la michezo ,rais wa ZFA ,katibu mkuu wa ZFA na mkurugenzi wa ufunzi wa ZFA wakifuatilia mazozei ya timu ya taifa ya Zanzibar asubuhi ya leo. |
Aidha amewataka wadau wa soka kuunga mkono juhudi za
chama chao ilikufanya maandalizi yakutosha kwa timu hiyo
Timu ya taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes)
inajiandaa na mashindano ya Afrika mashariki na kati yanayotarajiwa kufanyika
nchi Kenya mwishoni mwa mwezi huu nchini Kenya..