Tuesday, 25 April 2017

KHAMIS MUSSA ‘RAIS ‘ AIBEBA BOYS.

Khamis Mussa rais ameendeleza rekodi yake yakuwafunga mahasimu wao wa jadi ya Taifa Jang’ombe baada yakuifungia goli pekee la ushindi katika ushindi wa goli 1-0 mtanange uliovurumishwa katika dimba la Amani mjini Unguja usiku wakuamkia leo.

Katika mchezo huo ambao ulikuwa na ushindani wa hali ya juu na kuhudhuriwa na mashabiki lulkuki uwanjani hapo hadi timu zinaenda mapumziko hakuna timu iliyoona lango la mwenziwe.

Kurudi uwanjani kipindi cha pili kila timu ilifanya mabadiliko na mabadiliko hayo yaliinufaisha zaidi boys ambao walijiandikia goli hilo mnamo dakika ya 86 kutokana na kazi nzuri iliyofanya na Khamis Mussa.

Akizungumzia mchezo huo kocha msaidizi wa timu ya Jang’ombe boys Issa Amasha amesema mtanange huo ulikuwa nzuri na ushindani kwa pande zote nakuelezea kufurahishwa na ushindi huo.

Aidha kocha huyo amesema kuwa tayari timu yao imetinga katika hatua ya nane bora hivyo maandalizi yao kwa sasa nikuhakikisha timu inafanya vyema katika hatua hiyo nakutwaa ubingwa wa Zanzibar kwa msimu huu wa ligi.

Nae mwalimu wa timu ya taifa ya Jang’ombe Saleh Mussa Maisara amesema mchezo huo ulikuwa na ushindani kwa pande zote mbili lakini kutolewa kwa mchezaji wake kwa kadi nyekundu ndiko kulikopelekea kupoteza mchezo huo.

Aidha ameongeza kuwa wanarudi katika mazoezi kuyafanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza katika mchezo huo ilikufanya vizuri katika michezo miwili iliyosalia.

Kikosi cha timu ya Jang'ombe boys kilichoanza katika mchezo dhidi ya wapinzani wao wa jadi Taifa ya Jang'ombe



Kikosi cha timu ya Taifa ya Jang'ombe kilichoanza katika mchezo dhidi ya wapinzani wao wa jadi Jang'ombe boys .

BABU SHUBE ATOA SOMO KWA WAANDISHI

ALIYEKUWA kocha wa Timu ya Mdungu United Mohamed Shubeir, amesema ni jambo zuri kwa waandishi wa habari za michezo Kisiwani Pemba, kupatiwa taaluma hasa katika kipindi hiki cha Zanzibar kupata uwanachama wa CAF.

Alisema waandishi wa habari sasa wataweza kufanya kazi zao kwa umakini mkubwa, huku akiwataka makocha wenzake kuhakikisha wanatoa

mashirikiano kwa waandishi.

Shubeir aliyaeleza hayo wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa
habari hizi, katika uwanja wa michezo Gombani baada ya kumalizika kwa
mafunzo ya siku moja kwa waandishi wa habari juu ya CAF INTERCLUB
MEDIA GUIDELINS 2009.

“Waandishi wa Pemba wamekuwa wakikumbana na changamoto mbali mbali, zaidi kutoka kwa makocha wakati wanapotaka kufanya mahojiano nao, ni
jambo zuri sasa kwa makocha nao kupatiwa taaluma kama hiyo”alisema.

Aidha Shubeir alisema sasa wakati umefika kwa waandishi kuhakikisha
wanabadilika, katika uwandishi wao katika kipindi hiki Zanzibar
iliopata uwanachama wa CAF.

Alisema waandishi wanapaswa kuzisoma na kuzijuwa kwa kina kanuni za
shirikisho hilo, katika mashindano mbali mbali wanayoyasimamia ikiwemo
na ligi za nchi husika ili kuepuka kujakutia doa taifa.


Hata hivyo aliwataka makocha wenzake kubadilika kwa kwenda kufuata
taaluma za ukocha zaidi ili kuwendana na sheria na kanuni za CAF.

KIZIMKAZI YAMALIZA LIGI KWA USHINDI

TIMU ya Kizimbani imekamilisha michezo 32 katika ligi kuu ya Zanzibar,
baada ya kuitandika Younger Islander na kufikisha alama 61.

Kizimbani kwa sasa inaongoza ligi hiyo kwa muda, ikiwa mbele kwa alama
moja nyuma ya Jamhuri yenye alama 60 ikiwa na michezo 31 mkononi.
Mcheoz huo uliopigwa katika uwanja wa FFU Finya, huku ukishuhudiwa na
mashabiki wachache kiwanjani hapo, kutokana na timu hizo kumaliza
michezo yake.

Ushindi huo kwa Kizimbani umekuwa mchungu kwa Timu ya Younger Islandrambayo imeshuka hadi nafasi ya 13 katika ligi hiyo na kujihakikishia kushuka daraja.

Magoli ya Kizimbani yamefungwa na Ali Mkadam dakika 21, Mohamed Salim dakika 53 na Rajab Hafidh dakika 60, Younger Islander imefikisha alama 33 baada yakucheza michezo 32.

Kwa upande wa Ligi daraja la kwanza Taifa Pemba, Timu ya Cossovo
imetandika Nuru Boys goli 2-0, magoli ya washindi yamefungwa na Ali
Kheri dakika 21 na Abass Sultan dakika 58.


Timu ya Mkoroshoni na Muungano Ukombozi zimegawana alama 1-1, Uwanjani hapo.

RAIS ZFA AKABIDHI ZAWADI KWA WASHINDI KISIWANI PEMBA

RAIS wa Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA) Ravia Idarous Faina,
akikabidhi jezi na mipira miwili mmoja kati ya viongozi wa Timu ya
Elevan Star baada ya kuiba mshindi wa kwanza katika ligi daraja la
Tatu Wilaya ya Chake Chake.

Sunday, 23 April 2017

SERENGETI BOYS ‘YAWACHAPA’ GABON 2-1 MOROCCO, MKOKO AFUNGA GOLI LA USHINDI.

Mshambuliji wa timu ya Miembeni City Ibrahim Abdallah aliepo katika kambi ya timu ya taifa ya Tanzania ya vijana chini ya miaka 17 ameendeleza makali yake yakufumania nyavu baada yakuifuaingia timu hiyo goli la ushindi katika ushindi wa magol 2-1 dhidi ya Gabon.

Mshambuliaji wa timu ya Serengeti boys Ibrahim Abdallah (Mkoko) mwenye jezi namba 17 akishangilia goli na kiungo wa Asaad  
Katika mchezo huo wa kirafiki ikiwa ni miongoni mwa maandalizi ya timu hiyo kuelekea Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 Mkoko amejipatia goli hilo mnamo dakika ya 75 huku goli la kwanza likifungwa , Kelvin Nashon Naftali dakika ya 18
.

Akizungumza na zenjsport on line mshambuliaji wa timu ya Miembeni City Ibrahim Abdallah ambae yupo katika kambi hiyo ya Serengeti boys ameelezea kufurahishwa kwake na kiwango ambacho ameonesha katika mchezo huo nakusema kuwa anajipanga kuona anafanya vyema katika kila mchezo.

Aidha mshambuliji huyo amewataka wachezaji wenzake wa timu ya Miembeni City ambao wapo katika kambi kujiandaa na mchezo wao wa pili ligi daraja la kwanza taifa Unguja kuongeza bidii ya mazoezi huku akiwata kujutuma kwa nguvu zote nakupandisha timu ligi kuu.

Serengeti Boys imeweka kambi ya mwezi mmoja nchini Morocco kujiandaa na Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17, zinazotarajiwa kuanza Mei 14 hadi 28, mwaka huu nchini Gabon.


Huo unakuwa mchezo wa nne wa maandalizi kwa Serengeti kujiandaa fainali za Gabon, baada ya kuifunga Burundi mara mbili, Machi 30 mabao 3-0 na Aprili 1 mabao 2-0, mechi zote mbili zikipigwa Uwanja wa Kaitaba, Bukoba, kabla ya kulazimishwa sare ya 2-2 na Ghana ‘Black Starlets’ Aprili 3 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Serengeti Boys itakuwa kambini mjini Rabat hadi Mei 1, mwaka huu itakapowenda Younde, Cameroon kucheza mechi mbili za kirafiki dhidi ya wenyeji Mei 3 na 6, mwaka huu.
Mei 7 timu hiyo itakwenda Gabon ambako imepangwa kundi B pamoja na timu za Mali, Niger na Angola, wakati Kundi A lina timu za wenyeji, Gabon, Guinea, Cameroon na Ghana.

Wednesday, 19 April 2017

MAANDALIZI YOTE KUELEKEA MKUTANO MKUU ZFA YAKAMILIKA CHEUPE

Mkutano mkuu wa chama cha mpira wa miguu visiwani Zanzibar unatarajiwa kufanyika Jumamos ya April 22 katika kisiwa cha Pemba.

Akizungumzia maandalizi ya mkuutano huo mbele ya wanahabari afisa habari wa chama cha mpira wa miguu  visiwani Ali Bakar amesema maandalizi kwa ajili ya mkutano huo yanaenda vizuri.

Ameongeza kuwa kwa sasa chama chao kipo katika hatua za mwisho zakukalisha utoaji wa posho kwa wajumbe wa mkutano huo waliopo Unguja ili wakamilishe mahitaji muhimu ya familia zao.

Aidha amesema baadhi ya wajumbe wa mkutano huo wanatarajiwa kuondoka Ijumaa kuelekea kisiwani Pemba kwa usafiri wa baharini huku wengine wakitarajiwa kuondoa Jumamos kupitia usafiri wa angani.

Akizungumzia ajenda za mkutano huo amesema ajenda kuu ya kumtano huo ni mabadiliko ya katiba huku ajenda nyengine ndogondogo zikitarajiwa kujadiliwa katika mkutano.


Mkutano huo mkuu wa zararua unafanyika kufiatia ule uliofanyika katika kisiwa cha Unguja wiki tatu zilizopita unatarajiwa kufanyika katika ukumbi wa uwanja wa Gombani kisiwani Pemba.
AFISA HABARI WA CHAMA CHA MPIRA WA MIGUU VISIWANI ZANZIBAR ALI BAKAR ALI (CHEUPE)

Tuesday, 18 April 2017

Mkwasa ameelezea ‘picha’ la wachezaji wa Yanga kuachwa na ndege Algeria

Baada ya kuchapwa 4-0 na kuondoshwa kwenye michuano ya kombe la shirikisho Afrika, klabu ya Yanga ilipata pigo jingine kufuatia baadhi ya wachezaji pamoja na katibu mkuu Charles Boniface Mkwasa kuachwa na ndege baada ya kuchelewa kufika uwanja wa ndege.
Yanga walijikuta wameachwa na ndege baada ya kuchelewa kuripoti kwenye uwanja wa ndege kwa ajili ya kukaguliwa kabla ya safari, kundi la wachezaji 11 pamoja na Mkwasa walitakiwa kusafiri kwa ndege ya mchana lakini walifika uwanja wa ndege na kukuta ngege waliyotakiwa kusafiri nayo imeshaondoka.
Wachezaji wengine walifanikiwa kusafiri lakini ni wale waliotakiwa kuondoka kwa ndege ya jioni, Yanga walikwenda Algeria kwa makundi baada ya kushindwa kupata tiketi za pamoja kama timu, hivyo hata kurudi walipaswa kusafiri kama walivyokwenda.
Mkwasa ameelezea mkasa mzima wa tukio la kuachwa na ndege huku uhakika kurejea Tanzania ni hadi April 20, 2017.
“Baada ya kurudi kutoka kwenye mechi, tulipofika hotelini nilitanganza kwamba, kundi la wachezaji watakaoondoka mchana basi waondoke asubuhi baada ya chai (saa 2) waende uwanja wa ndege na kundi ambalo litaondoka mchana basi waondoke saa tano kwenda uwanja wa ndege.”
“Watu wakasema tutakaa sana uwanja wa ndege kwa hiyo bila kuangalia tiketi wakasema tuondoke saa tano kwenda uwanja wa ndege. Ilipofika saa nne tukaondoka kwenda uwanja wa ndege, kutoka tulipofikia hadi uwanja wa ndege ni parefu kidogo, tulipofika pale tukakuta milango imeshafungwa na ndege imeondoka na hakuna ndege yoyote.”
“Ndege iliyokuwepo ilikuwa tayari imeshajaa, na usafiri utakuwepo kuanzia tarehe 20, kwa kuwa na sisi tulisafiri kiutu uzima ikabidi turudi hotelini tuwapumzishe wachezaji tuwatafutie mahali pa kula na tunajaribu kufanya mawasiliano na wenzetu tuliocheza nao (MC Alger) kuangalia ni jinsi gani tunaweza kuishi lakini kiujumla ni kwamba hiyo ndio hali halisi ilivyokua.”
“Niseme tu kwamba, baada ya kutoka kwenye mechi watu wakawa wamechanganyikiwa ndio maana kulikuwa na hali ya ubishi wakashindwa kuelewa. Waliokuwa wanasafiri kwa usafiri mwingine bahati nzuri wao waliwahi lakini sisi kundi la watu 12 nikiwepo mimi tumebaki.”
Wachezaji walioachwa ni Kelvin Yondani, Deogratius Munishi ‘Dida’, Emanuel Martin, Thabani Kamusoko, Donald Ngoma, Haruna Niyonzima, Endrew Vicent ‘Dante’ Juma Abdul, Mwinyi Haji, Deus Kaseke, Ben Kakolanya pamoja na Mkwasa mwenyewe.
Mkwasa amethibisha kwamba, tayari wameshabadilisha tiketi na kupata zitakazowafanya wasafiri siku ya Jumatano April 19 na watafika Dar Alhamisi April 20, 2017.
Kwa mujibu wa ratiba ya ligi kuu Tanzania bara, Yanga wanatakiwa kucheza dhidi ya Tanzania Prisons April 22, 2017.

Mwamuzi wa Tanzania kuchezesha AFCON U-17 2017

Mwamuzi mtanzania Frank John Komba ni miongoni mwa waamuzi walioorodheshwa kuchezesha michuano ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 (U-17 Africa Cup of Nations) michuano ambayo imepangwa kufanyika Gabon.
Komba yupo kwenye orodha ya waamuzi wasaidi (Assistant Referees au washika kibendera) na ni mwamuzi pekee kutoka Tanzania aliyepata fursa hiyo kutoka Tanzania. Komba anaungana na waamuzi wengine wawili kutoka ukanda wa Afrika Mashariki Pacifique Ndabihawenimana (mwamuzi wa kati kutoka Burundi na Davies Ogenche Omweno (mwamuzi wa kati kutoka Kenya).
Orodha ya waamuzi watakaochezesha mashindano ya vijana nchini Gabon mapema mwezi ujao

MIEMBENI CITY ,YATUMA SALAMU KWA SEBLEN,YAILIPUA CHARAWE 2-0 .

Timu ya Miembeni City imeanza vyema kampeni yake yakutafuta tiketi yakucheza ligi kuu soka ya Zanzibar baada yakuifunga timu ya Charawe magol 2-0 katika mchezo wa hatua ya nne bora mtanange uliovurumishwa katika dimba la Amani mjini Unguja.

Katika mtanange huo ambao ulikuwa na ushindani kwa pande zote City wamejipatia magol yao kupiti Seif Salum Zola na Muhamed Vuai Prince.

Miembeni City ambayo imeeka kambi katika maeneo ya Fumba wilaya ya magharibi A Unguja itajitupa tena dimbani April 26 kumenyana na Seblem mchezo ambao unatarajiwa kuwa na ushindani kwa pande zote.

Matokeo hayo ya magol 2-0 waliyoyapata Miembeni City wanaendeleza rekodi yake yakutokupoteza katika michezo yake waliyokutana na Charawe ambapo timu hizo zimekutana mara saba Miembeni City wakishinda michezo sita huku wakitoka sare katika mchezo mmoja.
Walinzi wa timu ya Miembeni City Ali Mwinyi na Yussuf baada ya mchezo na Charawe mchezo ambao City imeibuka na ushindi wa magol 2-0.


Wachezaji wa Miembeni City wakiwasalimia washabiki wao kabla yakuanza mchezo kati ya timu yao na timu ya Charawe mchezo ambao City imeibuka na ushindi wa magol 2-0.

Wachezaji wa Miembeni City wakifuatili mchjezo kati ya timu ya Ng'ome na timu ya Seblen mchezo ambao Ng'ome waliibuka na ushindi wa magol 2-1