Monday, 5 June 2017

Miembeni City yatema sita kusajili kumi wapya.


Bodi ya wakurugenzi ya timu ya Miembeni City imekutana jioni ya jana kupitia ripoti ya mwalimu sambamba na kujadili masuala kadhaa yahusuyo timu ikiwa na suala la usajili kwa ajili ya msimu ujao wa ligi.

Wachezaji wa Miembeni City wakiingia uwanja.
Katika kikao hicho bodi hiyo imeipitia riport ya mwalimu aliyowasilisha nakuungana na mapendekezo ya mwalimu yakuacha nyota sita nakuongeza wengine kumi kulingana na nafasi alizopendekeza mwalimu.

Akizungumza na mtandao huu mkurugenzi wa ufundi wa timu hiyo Ali Muhamad amesema  wajumbe wa bodi ya wakurungezi wa timu imerizia mapendekezo ya mwalimu ikiwemo kuacha nyota wao sita huku wakiongeza wengine kumi wapya.
Nyota wa Miembeni City.


“Ni kweli bodi imekubaliana na ripoti ya mwalimu na kwa sasa tupo katika kuyafanyia kazi mapendekezo ya mwalimu ikiwemo kuacha nyota hao sita huku nyota wawili tukiwaeka sokoni kutokana na mikataba yao kuwa ya muda mrefu katika timu yao hiyo”alisema mkurugenzi huyo waufundi.

Akiwataja nyota ambao watawaacha katika kikosi chao ni pamoja na Khamis Hamad Muhamed,Khamis Muhamed Ali,Yussuf Mussa kheri,Ali Muhamed Juma,Yussuf Dotto Shaaban na Yussuf Kassim Yussuf.
Nahodha wa timu ya Miembeni City Habibu Ali


Ameongeza kuwa wachezaji Adam Khamis Mohamed na Farid Uled Wadi wamewaeka sokoni kwa timu ambayo itawahidi kufanya mazungumzo na uongozi wa timu hiyo.

Amefafanua kuwa wapo katika mazungumzo na baadhi ya nyota kuwajumuisha katika kikosi chao na endapo watafikia makubaliano nakufungana nao mkataba watawaeka wazi nyota.


Mkurugenzi wa ufundi wa Miembeni City akiwa na mlinzi wa timu hiyo Abubakary Ame.


Kuhusu kutakiwa kwa baadhi ya nyota wake na timu nyengine zinazocheza ligi kuu soka ya Zanzibar mkurungezi huyo amesema uongozi wa timu haujapata ofa mpaka sasa kutoka timu yoyote na endapo itatokea watakaa nao mezani kuona uwezekano wakufanya mazungumzo na timu hiyo.

No comments:

Post a Comment