Monday, 31 July 2017

Bushir aeka wazi sababu zilizomfungisha virago Mwadui FC.



Aliyekuwa kocha mkuu wa timu ya Mwadui FC Ali Bushir Mahmoud ameelezea sababu iliyopelekea kuondoshwa kukinoa kikosi hicho.
 
Aliyekuwa kocha wa Mwandui FC Ali Bushir Mahmoud.

Akizungumza na mtandao huo kocha huyo amesema amepokea barua yakumjulisha kuondolewa kuitumikia kikosi hicho July 27,mwaka huu iliyoandikwa na katibu mkuu wa timu hiyo.

Amesema kuwa katika barua hiyo imeelezea sababu kuu tatu ambazo zimemfanya afukuzwe kuinoa timu hiyo ambazo nikutokuwa na mashirikiano na wachezaji wa timu hiyo,viongozi pamoja na benchi la ufundi hususani kocha msaidizi wa timu hiyo.

Akielezea sababu nyengine ni timu kutokushinda mchezo hata mmoja wa ugenini tokea kuichukua timu hiyo ambapo ilicheza michezo saba ya ugenini nakupoteza huku michezo saba kati ya nane waliocheza nyumbani wakishinda.

Amesema kuwa sababu nyengine ambayo imepelekea kuondoshwa katika kikosi chake ni migogoro iliyopo kati yake na wachezaji wa timu hiyo.

Ameongeza kuwa sababu ambazo zimeelezwa na uongozi wa timu hiyo haziingii akilini kwa vile kama utaziangalia kwa undani na namna timu ilivyopata matokeo mazuri. 

“ Hizi sababu kusema ukweli haziingii akilini kwa sababu niliichukua timu ikiwa nafasi ya tatu kutoka mkiani sasa kama ingekuwa hakuna mashirikiano kati yangu na wachezaji sambamba na uongozi basi tusingeweza kupata matokeo mazuri nakuibakisha ligi ikiwa ligi kuu”alisema kocha huyo.

Ameogeza kuwa kwa sasa anajiandaa kupokea mafao yake kutoka timu hiyo huku akisema kuna ofa kadhaa ameshazipata kutoka timu mbalimbali zinazoshiriki ligi kuu ya soka ya Tanzania bara.

Katikati ya msimu uliopita Bushir alichukua mikoba ya Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ na kujiunga na Mwadui FC ambapo aliikuta timu hiyo ipo nafasi ya tatu kutoka chini na kufanya kazi kubwa mpaka kuisadia kuinusuru kushuka daraja.

No comments:

Post a Comment