Serikali ya
mapinduzi ya Zanzibar kupitia wizara ya habari utamaduni utalii na
michezo,baraza la michezo ,wizara ya elimu na mafunzo ya amali kwa kushirikiana
na chama cha mpira wa miguu visiwani ZFA vimeshauriwa kuelekeza nguvu zao katika kusaidia na kuendeleza michezo kwa
vijana ilikutengeza taifa lililobora kimichezo.
 |
Mshambuliaji wa Serengeti boys Ibrahim Abdallah Mkoko akiwa katika majukumu ya taifa . |
Ushauri huo
umetolewa na mshambuliaji wa timu ya taifa ya vijana ya Tanzania ya chini ya
miaka 17 Serengeti boys Ibrahim Abdallah(Mkoko) wakati alipokuwa akizungumza na
mtandao huu nakusema kuwa endapo serikali na wadau wakuu wa michezo wataekeza
kuanzia chini Zanzibar itatajika kwa michezo kimataifa.
Amesema nchi
zote ulimwenguni ambazo zimepiga hatua kimichezo wameekeza kwa vijana jambo
ambalo limeweza kuzisaidia nchi hizo kiuchumi.
 |
Baadhi ya vijana wakizanzibar wakionesha uwezo wao wakusakata kabumbu. |
Ameongeza
kuwa Zanzibar imebahatika kuwa na vijana wengi wenye vipaji katika michezo
mbali mbali lakini kutokuwepo kwa sera nzuri yakukuza,kuendeleza na kuimarisha
vipaji vya vijana hao ndiko kunakopelekea kudumaa kwa vipaji vya vijana hao.
Amepongeza mpango
wa wizara ya elimu wakuwa na mfumo wa mashindano ya elimu bila malipo ambayo
husirikisha wanamichezo kutoka shule mbalimbali za msingi na sekondari nakutoa
nafasi kwa vijana kuonesha uwezo wao,nakushauri vijana ambao wataonesha vipaji
katika michezo hiyo kuendeleza zaidi ilikuepusha kudumaa kwa vipaji walivyo
navyo.
“ Huu
utaratibu unaofanya na wizara ya elimu wakuandaa haya mashindano ya elimu bila
ya malipo ni nzuri lakini uwepo mpango wakukusanywa wale wote wenye uwezo
ilikuendelezwa vipaji walivyonavyo ili visije kupotea”Alisema Mkoko.
Kuhusu
Zanzibar kupatiwa uwanachama wa shirikisho la soka barani Afrika (CAF) Mkoko amesema
ni jambo jema na litasaidia kutoa fursa kwa vijana wakizanzibar kujitangaza
huku akikiomba chama cha mpira wa miguu visiwani kuanza maandalizi ya mapema
kwa timu zake ambazo huenda zikaanza kushiriki katika mashindano mbalimbali
yanayoandaliwa na shirikisho hilo.
“Nimefarijika
sana Zanzibar kupata uanachama wa shirikisho la soka barani Afrika huu ni
wakati wa vijana wa kizanzibar kutangaza vipaji vyao kimataifa jambo la msingi
na la umuhimu nikwa chama cha mpira wa miguu visiwani Zanzibar kuanza
maandalizi ya timu zake mapema ilikuona wanafanya vyema katika mashindano
wakati utakapowadia”Alisema.
Akizungumza malengo
yake katika soka Mkoko amesema ndoto zake ni kucheza soka lakulipwa lakini kwa
sasa atahakikisha anafanya mazoezi kwa bidii kuona anaisadia timu yake anayochezea
kwa sasa.
“Unajua
lengo nikucheza soka la kulipwa nje ya Tanzania lakini ili upate nafasi
yakufika huko lazima ufanye bidii katika mazoezi,uwe na nidhamu ya hali ya juu
nakujituma katika mashindano,kwa sasa naaendelea kujinoa kwa ajili ya haya
mashindano ya Rolling Stone lakini nikirudi huko nitaelekeza nguvu zangu katika
timu yangu,unajua msimu uliomalizika sijapata kuitumikia sana kilabu yangu kwa
vile nilikuwepo katika kambi ya timu ya taifa lakini msimu huu nitahakikisha
naisaidia timu yangu kwa nguvu zangu zote”Alimaliza Mkoko.